Nyamagana kumekucha,uwekaji nyasi bandia waanza rasmi


Hatua za awali za ukarabati kuelekea uwekaji wa nyasi bandia kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana Jijini Mwanza unaendelea vizuri ambapo leo ni siku ya pili tokea zoezi hilo lianze.

ukarabati wa uwanja wa nyamagana
Uwanjwa wa Nyamagana katika ukarabati

Wakuganda in sports imeshuhudia hii leo asubuhi jinsi  Jassie and Company Limited ( JASCO) ambayo imepewa kazi hii ya ukarabati wa uwanja huo,  ikiendelea  vema ikiwa ni pamoja na kazi ya kuchimba udongo sehemu ya kuchezea (Pitch)
Kampuni ya ukarabati uwanja wa Nyamagana-JESCO
Kwa mujibu wa kampuni ya ushauri wa kitaalamu (ACT Global Consultancy) ya nchini Marekaniambayo inasimamia zoezi hilo kwa niaba ya shirikisho la soka ulimwenguni – FIFA, zoezi linakwenda vizuri na wananchi wa Mwanza na Tanzania kwa ujumla wasubirie kuona uwanja wa Nyamagana ukiwa kwenye hadhi ya kipekee.
“Sisi tuko makini na hatuna mchezo kwenye kazi. Tunasimamia ujenzi huu na kupeleka taarifa FIFA. Tutahakikisha tunafanya kazi hii vizuri ili kujijengea kupata kazi zingine FIFA” amesema mmoja wa wahandisi wa kampuni ya ACT  Global  Bibonimana Dieudonne.
Aliongezea kuwa  katika hatua za awali miongoni mwa kazi zitakazotekelezwa ni kuchimba udongo, kuweka changarawe, kuweka kokoto, kushindilia udongo,kuweka mabomba kwa ajili ya kupitisha maji.
Hii sio mara ya kwanza kwa kampuni hiyo chini ya mpango wa FIFA Goal Project kufanya kazi ya ushauri wa kitaalam kwani tayari kwani tayari imesimamia ujenzi wa viwanja chi za Chad, Misri, Malawi, Burundi,Jamhuri ya kidemocrasia ya Kongo.
Bibomana ameahidi kuwa ndani ya miezi miwili kazi ya uwekaji wa nyasi bandia itakuwa imekamilika endapo tu kama FIFA itatumia wajibu wake kwa kutuma pesa kwa wakati sambamba na vifaa.

isaack wakuganda akihojiana na Bibonimana
Isaacki wakuganda-wakuganda in sports (kushoto) akihojiana na Bibonimana Dieudonne
(mhandisi kutoka kampuni ya ACT Global Consultancy)

Siku za hivi karibuni yalibuka maswari mengi kuhusu uwekaji wa nyasi bandia kwenye uwanja wa huo kutokana na zoezi hilo kuchukua muda mrefu bila mchakato wake kuanza. Lakini sasa kila kitu kiko wazi.

Uchimbaji udongo katika uwanja wa Nayamagana
Uchimbaji udongo katika uwanja wa Nyamagana

Ili kufanikisha zoezi hilo la Uwekaji wa nyasi bandia katika Uwanja huo wa Nyamagana, FIFA ilitoa kiasi cha dola za Marekani 500,000 ambapo Halmashauri ya Jiji la Mwanza ambao ndiyo wamiliki wa uwanja huo, imechangia kiasi cha dola 118,000 (Sh milioni 295) kama mchango wake kwa ajili ya zoezi hilo ambalo linatarajiwa kugharimu dola 618,000 (Sh milioni 988).


Uchimbaji wa udongo - Nyamagana
Zoezi la uchimbaji udongo - uwanja wa Nyamagana

Uwanja wa Nyamagana utakuwa ni uwanja wa nne kuwekewa nyasi hizo za bandia hapa nchini ambapo tayari viwanja vya Uhuru na Karume vya jijini Dar es Salaam na Migombani cha Zanzibar vimewekewa nyasi hizo huku Uwanja wa Kaitaba Mkoani Kagera nao ukiwa ni Miongoni mwa Uwanja ulio katika orodha ya kuwekewa nyasi bandia na hivyo kuongeza idadi ya viwanja vyenye nyasi bandia hapa nchini.


Ukarabati wa uwanja wa Nyamagana-ofisi za chama cha soka wilaya ya Nyamagana
Ofisi ya chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Nyamagana

Share on Google Plus

About Unknown

"Is the CEO and Co-Founder of wakuganda in sports blog, dedicated to give you Sport roundups, updates, live scores and all sporting events,"
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment