Sare dhidi ya Coastal yaipeleka Simba Zanzibar

Uongozi wa klabu ya Simba umesema sare ya mabao 2-2 dhidi ya Coastal Union, jana, haukuwa mzuri kwao lakini wameupokea kama changamoto.

Geofrey Nyange - Simba
Geofrey Nyange, Makamu Rais wa Simba
Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amesema wanaichukulia sare hiyo kama changamoto na sehemu ya kujipanga.
“Hakuna aliyetarajia, inawezekana vijana wetu walijisahau baada ya kuongoza kwa mabao mawili wakaona tumeshinda.
“Kipindi cha pili Coastal Union wakajirekebisha na kucheza mchezo mzuri na kutupa wakati mgumu, mwisho wakasawazisha,” alisema Kaburu.
“Tayari tumeanza kambi Zanzibar na tutayatumia makosa ya mechi iliyopita kama sehemu kujiimarisha.”


Simba itacheza mechi ya pili dhidi ya Polisi Morogoro katika mechi itakayopigwa Jumamosi ijayo.
Share on Google Plus

About Unknown

"Is the CEO and Co-Founder of wakuganda in sports blog, dedicated to give you Sport roundups, updates, live scores and all sporting events,"
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment