Pepsi Kombe la Meya Kuhitimishwa leo

Stanslaus Mabula (wa pili kutoka kushoto) mstahiki Meya wa halmashali ya jiji la Mwanza akikabidhi vifaa kwa ajili ya pepsi - meya cup

Mashindano ya soka ya Pepsi kombe la Meya yatafikia tamati join ya leo kwa mtanange wa fainali kupigwa kwenye dimba kongwe la Nyamagana jijini Mwanza kati ya timu ya kata ya Mkolani na ile ya kata ya Mirongo.
Mchezo huo wa fainali utatanguliwa na mchezo wa kutafuta nafasi ya tatu ambao utazikutanisha timu za Mnadani na Sokoni.
Kwenye fainali ya leo, Mkolani wanaonekana kupania zaidi kutwaa ubingwa wa mashindano hayo kwani mwaka jana pia ambapo mashindano hayo yalianza, Mkolani ilitinga fainali na kubamizwa na isamilo kwa mabao 2 – 1
Akizungumza na isaackwakuganda.blogspot.com asubuhi ya leo, Mratibu wa mashindano hayo Mohammed Bitegeko amesema kuwa , matayarisho yote kuelekea fainali ya leo yamekamilika huku pia akisema kuwa mashindano ya mwaka huu yamekuwa bora zaidi ya yale ya mwaka jana
“Kiukweli mashindano yet yamekuwa mazuri sana, kwanza tuliongeza idadi ya viwanja vilivyotumika  ambapo tumetumia viwanja sita , tumetoa vifaa vingi vya michezo kwa timu shiriki lakini kizuri zaidi tumetumia waamuzi Kutoka kituo cha kukuza vipaji vya michezo cha Alliance jijini Mwanza” amesema Bitegeko.
Zawadi za washindi wa mashindano ya pepsi kombe la Meya kwa mwaka huu ni
Mshindi wa 01
  • Bajaji ya kisasa ya mizigo thamani ml 4.5
  • TSH. Ml 1.5
  • Kombe
  • Medali za dhahabu

Mshind wa 02
  • TSH mil 3
  • Medali za fedha

Mshindi wa 03
  • TSH mil 2
  • Medali za shaba

Timu yenye nidhamu
  • Itaambulia THS 200,000/=

Mfungaji bora
  • TSH 200,000/=

Mwalimu Bora
  • TSH 200,000/=

Mashindano hayo yamefanyika kwa mara ya pili mwaka huu yakishirikisha jumla ya timu 22 kutoka wilaya ya Nyamagana kutoka kata 12 za jimbo la Nyamagana na timu 10 kutoka katika makundi maalum
Mashindano yalianza Agosti 02,2014 yakiwa chini ya udhamini wa kampuni ya SBC Tanzania Limited kupitia kinywaji cha cha Pepsi, huku muasisi wa mashindano hayo akiwa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya jiji la Mwanza ambae pia ni diwani wa kata ya Mkolani  - Stanslaus Mabula




Share on Google Plus

About Unknown

"Is the CEO and Co-Founder of wakuganda in sports blog, dedicated to give you Sport roundups, updates, live scores and all sporting events,"
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment