LIGI KUU ENGLAND,VIWANJA KUWAKA MOTO

Ligi Kuu ya England inaendelea leo katika viwanja mbalimbali, huku kila timu ikisaka pointi tatu muhimu katika msimamo wa ligi hiyo.

mshambuliaji wa Liverpool "Super" Mario Baloteli

 

Katika mchezo wa mapema Jumamosi, Liverpool watakuwa wageni Newcastle katika mpambano huo. Katika rekodi za nyuma Liverpool haijawahi kushindwa dhidi ya Newcastle katika mechi nne walizokutana, Liverpool wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi nyingine mbili. Hata hivyo hakujawahi kutokea sare ya bila kufungana kati ya timu hizi katika mapambano 40 ya Premier League. Kwa mara ya kwanza sare ya kutofungana kati ya Liverpool na New Castle ilikuwa mwezi Februari 1974.

Timu ya Newcastle ilipoteza wachezaji watano kwa kupigwa kadi nyekundu katika michezo minne waliyokutana na Liverpool.
Katika michezo tisa iliyochezwa na timu hizo katika ligi kuu ya England inayoendelea, Liverpool inashika nafasi ya saba ikiwa na pointi 14, huku Newcastle ikiwa katika katika nafasi ya 14 na pointi 10.
Michezo mingine ya Jumamosi ni kati ya Arsenal na Burnley, Chelsea dhidi ya QPR, Everton wakimenyana na Swansea, Hull wakipepetana na Southampton, Leicester wakionyeshana kazi na West Brom, huku Stoke City wakinyukana na West Ham.

Kati ya michezo itakayochezwa Jumapili, mechi inayosubiriwa na mashabiki wengi duniani ni kati ya Manchester City watakapovurugana na ndugu zao Manchester United. Manchester City wanashikilia nafasi ya tatu wakiwa na pointi 17, huku Manchester United wakiwa nafasi ya nane na pointi 13.
Mchezo mwingine ni kati ya Aston Villa na Tottenham.

Share on Google Plus

About Unknown

"Is the CEO and Co-Founder of wakuganda in sports blog, dedicated to give you Sport roundups, updates, live scores and all sporting events,"
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment