TOTO AFRICANS YAZIDI KUJIKITA KILELENI LIGI SOKA DARAJA LA KWANZA

Klabu ya soka ya Toto Africans ya Mwanza ,imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi soka daraja la kwanza[FDL]kwa upande wa kundi B baada ya hapo jana kutoka sare ya kufungana bao 1-1 na Polisi Mara kwenye dimba la Karume mjini Musoma mkoani Mara

Nahodha wa Toto African (Kulia) akisalimiana na nahodha wa Polisi Mara Katika mchezo wao wa kwanza dimba la CCM Kirumba

Kwa matokeo hayo,Wana- Kishamapanda hao wamefikisha alama 16 hivyo kuendelea kubaki kileleni baada ya kucheza michezo minane.Michezo mingine iliyochezwa hapo jana imeshuhudia sare kutawala ambapo  kwenye uwanja wa Ushirika mkoani Kilimanjaro,wenyeji Panone Fc wametoka sare ya mabao 2-2 na JKT Oljoro  huku Polisi Tabora ikitoka sare ya 0-0 na Rhino Rangers kwenye dimba la Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora

Michezo mingine mitatu ya kundi B itachezwa leo ambapo Geita Gold Sc itaikaribisha Green Warriors kwenye uwanja wa Nyankumbu  sekondari huku Mwadui Fc ikiikaribisha JKT Kanembwa kwenye dimba la Mwadui mkoani Shinyanga.Wafunga buti wa Polisi Dodoma watakuwa nyumbani Jamhuri mkoani Dodoma kucheza na Burkina Faso Fc ya mkoani Morogoro
Timu mbili zitakazoshika nafasi za juu kwenye kundi B na mbili kutoka kundi A-zitafuzu kucheza Ligi kuu soka ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa mwaka 2014/2015
Share on Google Plus

About Unknown

"Is the CEO and Co-Founder of wakuganda in sports blog, dedicated to give you Sport roundups, updates, live scores and all sporting events,"
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment