Klabu ya soka ya Toto Africans imefanikiwa kurejea kileleni mwa kundi B la ligi soka daraja la kwanza baada ya hapo jana kuizamisha JKT Oljoro ya mkoani Arusha kwa mabao 3-1 kwenye dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza
![]() |
| Kocha mkuu wa Toto Africans John Tegete akitoa maelekezo kwa wachezaji wake wakati wa mapumziko hapo jana |
Wana-Kishamapanda walianza kuzifumania nyavu za wapinzani
kunako dakika ya 19 kwa bao la penati
lililofungwa na Emmanuel Swita ambaye
shuti lake lilimshinda mlinda mlango Amani Simba na kutinga nyavuni
Penati hiyo ilitolewa baada ya nyota wa mchezo wa jana kwa
upande wa Toto,Hamim Abdul Karim kufanyiwa madhambi kwenye eneo la hatari na
mlinzi wa JKT Oljoro Yusuph Machogote
JKT Oljoro baada ya kufungwa bao hilo iliongeza kasi ya mashambulizi
langoni mwa Toto Africans na katika
dakika 28 ilifanikiwa kusawazisha
bao kwa njia ya penati kupitia kwa Swalehe Hussein baada ya Ally Ahmed
kuangushwa kwenye eneo la hatari na Miraji Maka
Toto Africans ilifunga bao la pili dakika ya 40 kupitia kwa
Hamim Abdul Karim aliyefunga kwa shuti kali kufuatia majalo nzuri kutoka winga
ya kulia iliyopigwa na Severine Constantine
Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika,Toto
Africans ilikuwa mbele kwa mabao 2-1
Nyota wa mchezo wa jana kwa upande wa Toto Africans,Hamim
Abdul Karim katika dakika ya 68
aliifungia Toto bao la tatu baada ya majalo nzuri kutoka winga ya kushoto
iliyopigwa na kiungo mkongwe Emmanuel Swita
Hadi filimbi ya mwisho ya mchezo huo inapulizwa,Toto
Africans iliondoka na ushindi wa pointi zote tatu na hivyo kuongoza ligi daraja
la kwanza kwa kundi B baada ya kufikisha alama 19 katika michezo tisa huku
Mwadui FC ya Shinyanga ikiporomoka hadi nafasi ya pili ikiwa na alama 17 lakini ina michezo minane
Baada ya mchezo wa jana,Kocha mkuu wa Toto Africans John
Tegete alisema kuwa amefurahishwa na kiwango ambacho wachezaji wake walikionyesha hapo jana huku akimwagia
sifa nyingi mshambuliaji Hamim Abdul
Karim ambaye alifunga mabao mawili
‘Nimefurahishwa sana na haya matokeo,kama umeangalia vizuri
kikosi changu kimeimarika.Nimefanya marekebisho kwenye safu ya ushambuliaji
ambapo,Hamim Abdul Karim kwenye michezo iliyopita nilikuwa nikimchezesha kwenye
nafasi ya ulinzi lakini leo amecheza kwenye ushambuliaji na kufunga mabao
mawili na sasa ana jumla ya mabao manne,ni mchezaji mwenye uwezo wa hali ya
juu.Nawaambia wakazi wa Mwanza watarajie kuiona timu yao ikitinga Ligi kuu soka
Tanzania Bara msimu ujao na nawaahidi kuwa mchezo wetu ujao wa Jumatano ijayo
dhidi ya Geita Gold SC tutaibuka na ushindi mzuri’alisema Tegete
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea hii leo kwa michezo mitano
kuchezwa ambapo JKT Kanembwa itaikaribisha Polisi Tabora kwenye uwanja wa Lake
Tanganyika,Mwadui FC Shinyanga itakuwa mwenyeji wa vibonde Green Warriors
kwenye uwanja wa Mwadui,Wafanyabiashara wa mafuta-Panone FC
watakua wenyeji wa Geita Gold SC kwenye uwanja wa Mwadui
Burkina Faso ya Morogoro itakua mgeni wa Rhino Rangers
kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora huku Polisi Dodoma watakua
mwenyeji wa Polisi Mara

0 comments:
Post a Comment